Repository logo
  • English
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • Latviešu
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Қазақ
  • বাংলা
  • हिंदी
  • Ελληνικά
  • Yкраї́нська
  • Log In
    New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
Repository logo
  • Communities & Collections
  • All of DSpace
  • English
  • Català
  • Čeština
  • Deutsch
  • Español
  • Français
  • Gàidhlig
  • Italiano
  • Latviešu
  • Magyar
  • Nederlands
  • Polski
  • Português
  • Português do Brasil
  • Suomi
  • Svenska
  • Türkçe
  • Tiếng Việt
  • Қазақ
  • বাংলা
  • हिंदी
  • Ελληνικά
  • Yкраї́нська
  • Log In
    New user? Click here to register.Have you forgotten your password?
  1. Home
  2. Browse by Author

Browsing by Author "Kinoti, Timothy M."

Now showing 1 - 11 of 11
Results Per Page
Sort Options
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Dhima ya Kiswahili katika Uimarishaji wa Utamaduni na Mazingira kwa Mujibu wa Katiba ya Kenya
    (East African Scholars Publisher, 2019-09) Kinoti, Timothy M.
    The Constitution of the Republic of Kenya recognizes culture and environment as important pillars upon which the identity of its people is anchored. Chapter Two, Section 11 of the Constitution takes cognizant of culture as the foundation of the Nation and as the cumulative civilization of the Kenyan people and nation. The Constitution expressly states that the State shall promote all forms of national and cultural expression through literature, the arts, traditional celebrations, science, communication, information, mass media, publications, libraries and other cultural heritage. It also recognizes the role of science and indigeneuos technologies in national development and also the promotion of the intellectual property rights of the people of Kenya. This paper discusses the role of Kiswahili language and literature in cultural and environmental conservation, which are key indicators of development of any civilized society. Kiswahili is constitutionally recognized as the national and official language in Kenya.
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Kiswahili Poetry and Its Role in Preservation of the History of Struggle for Freedom in Africa
    (2015) Kinoti, Timothy M.; Kobia, John M.; Mukuthuria, Mwenda
    This research investigated the portrayal of the African politician in Kiswahili poetry. Basically, this research intended to shed light on how different poets have portrayed African politicians creatively with a purpose of revealing how these leaders have changed since colonial times to the multi-party period. The research assumed that political leaders played a great role in the development of their individual countries and Africa as a whole. The attainment of various developmental goals such as Kenya’s Vision 2030 and strengthening of the East African Community is to a large extent pegged on political decisions. The objectives of this research were to investigate the role of Kiswahili poetry in preserving the history of the African politician and to examine the traits of the pre-colonial and post-colonial African politician according to Kiswahili poets. The researcher assumed that the poet speaks for the citizen who gets adversely affected by decisions and actions taken by politicians. The study was guided by Romanticism theory developed by William Wordsworth and Samuel Taylor Coleridge and Post-colonial Theory which is associated with the works of Edward W. Said, Gayatri Chakravorty Spivak and Homi K. Bhabha. The study was carried out in the library where purposive sampling method was used to collect data from selected anthologies. Qualitative analysis of the selected poems was done guided by the research objectives. The findings of this study revealed that Kiswahili poetry is an important tool for preserving the history of Africa’s struggle for independence. The study also revealed how the seemingly royal pre-independence African politician changed drastically after independence was attained and became a tormentor of the very people he had sworn to protect. Despite these shortcomings, it is evident that the African continent has a few political role models whom the current and future politicians can emulate. The findings of this research will benefit Kiswahili scholars, writers and all political stakeholders in Africa and beyond.
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Mchango wa Lugha za Kiasili katika Uafikiaji wa Maendeleo Endelevu
    (2021-06) Kinoti, Timothy M.
    Makala hii inajadili dhima ya lugha za kiasili, ikiwemo ya Kiswahili, katika kuafikia maendeleo endelevu barani Afrika. Kimsingi, asilimia kubwa ya wenyeji wa bara hili huishi katika maeneo ya mashambani na huzitumia lugha za kiasili katika mawasiliano ya kila siku. Kati ya sekta muhimu zinazoathiriwa na matumizi ya lugha ni pamoja na elimu, habari na mawasiliano, burudani, dini, uandishi na uchapishaji, utunzaji na uhifadhi wa mazingira, afya, kilimo na biashara. Aidha, upatikanaji wa maendeleo endelevu utategemea kwa kiasi kikubwa iwapo wananchi watashirikishwa katika aina mbalimbali za utafiti na matokeo yake kuwasilishwa kwa lugha wanayoielewa ili waweze kuyatekeleza. Makala hii inachukulia kuwa lugha inayo dhima kuu katika utekelezaji wa huduma na shughuli mbalimbali za kitaaluma.
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Portrayal of the Contemporary African Politician in Swahili Poetry
    (2015-09) Kinoti, Timothy M.; Mwenda, Mukuthuria; Kobia, John M.
    This study was, in a broader sense, intended to identify the many political, social and economic changes that the continent of Africa has undergone since independence. Among the significant changes witnessed are those of its political leaders. This study analyzed the various traits and actions of Africa’s contemporary political leaders as portrayed by Kiswahili poets. The objective of this study was to evaluate the changes that the contemporary African politician has undergone since the attainment of multiparty democracy according to swahili poets. The study was guided by post-colonial Theory which is associated with the works of Edward W. Said, Gayatri Chakravorty Spivak and Homi K. Bhabha. Data was collected from selected onthologies of Kiswahili poems using purposive sampling method. Qualitative analysis of the selected poems was done guided by the research objective. The findings of the study revealed that although the African continent has made remarkable steps in enhancing democracy, a good number of its political leaders, whom were credited for championing multiparty democracy, have turned out to be tormentors of the very people they had sworn to protect
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Proceedings from the first Annual International Conference on Decolonizing Education
    (University of Embu, 2020-02) Kenya, Eucharia U.; Njiruh, Nthakanio P.; Gitonga, Ciriaka; Muturi, Margaret; Kinoti, Timothy M.; Njagi, Zachary
    Decolonizing formal education involves accepting indigenous and alternative ways of envisioning the world around us. For academics, it would entail accepting indigenous perspectives, ways of knowing and wisdom, and encouraging efforts by staff and students alike to reclaim indigenous knowledge as well as philosophies of teaching and learning that encompass the multiple experiences of a people. In higher education, such shift is important not only for pedagogic reasons, but also as an important part for example in African studies. On a positive note, recent developments have seen a paradigm shift and ‘detachment’ from the concept of pure formal education. Agitation for recognition of the indigenous concepts, ideas and innovations in enhancing and tackling challenges affecting humanity, whether from developing or developed countries, is like a stone rolling downhill with minimal barriers that must reach its destination. To begin a conversation geared towards drawing a roadmap for decolonizing African education, the 1st Annual International Conference on Decolonizing Education sought to examine knowledge production and resistance to colonial and post-colonial domination. Together, scholars, researchers, practitioners, elders, community leaders, community/digital/ media activists and artists, and educators engaged in a dialogue on (re)claiming and use of indigenous pedagogies as tools for response to colonial fragmentations. The three-day event prevailed upon participants to strengthen and build more confidence in indigenous knowledge, ideologies, philosophies, mechanisms and customs for continued eradication of colonial mindsets. It indeed endeavored to address human, political orientation, the triggers and factors that sustain the belief that indigenous knowledge, customs and beliefs are of less importance in shaping our destiny and that of the globe.
  • No Thumbnail Available
    Item
    Ubadili Maana katika Leksia za Kîîtharaka: Mtazamo wa Kifonolojia na Kimofolojia
    (2022) Mwembu, Kimathi; Mugambi, Allan; Kinoti, Timothy M.
    Makala haya yanalenga kubainisha jinsi ubadili katika vitamkwa na mofu unavyoathiri maana ya leksia katika Kîîtharaka. Maana katika leksia hutegemea kipengele cha kiisimu na vile vile kile cha kijamii ili ieleweke vilivyo. Katika hali hii, mabadiliko ya kifonolojia, kimofolojia, pamoja na kileksia yanayoathiri maana yameangaziwa. Data ya kimsingi kutoka wazungumzaji asilia wa Kîîtharaka, imechanganuliwa kwa kutumia nadharia ya Leksika-Pragmantiki. Makala haya yanabainisha ubadili wa kifonolojia pamoja na kimofolojia ambao huchangia katika kuibuka kwa maana fulani katika leksia za Kîîtharaka. Makala haya yanabainisha kwamba maana katika leksia za Kîîtharaka hutegemea kwa njia moja au nyingine mabadiliko yanayohusisha usilimisho, kuimarika na kudhoofika kwa fonimu, uchopekaji, uyeyushaji, hapololojia, kanuni ya Dahl na Ganda. Aidha, ubadili unaoathiri maumbo ya mofu huchangia pakubwa kutokea kwa maana katika leksia. Mofu za ngeli, ukanusho na uambishaji ni miongoni mwa zile ambazo zimebainika kuathiriwa na ubadili, ambao huzua maana fulani. Makala haya yanahitimisha kwamba, maana ya leksia huwa na misingi yake katika kiwango cha fonimu na mofimu zinazotumika kuunda neno. Pia, kuna mwingiliano baina ya maana kimatumizi na maana kimuktadha wa leksia..
  • No Thumbnail Available
    Item
    Ubainishaji wa vigezo vya Utoaji Wa Toponemia katika Jamii: Mfano kutoka Jimbo Dogo la Maara nchini Kenya
    (2022) Mutegi, David Micheni; Mugambi, Allan; Kinoti, Timothy M.
    Utafiti huu wa kionomastiki ulilenga kuchanganua vigezo vya utoaji wa toponemia za shule za msingi katika jamii. Utafiti ulifanyika katika eneo la Mwimbi na Muthambi, jimboni dogo la Maara kwenye Kaunti ya Tharaka-Nithi, nchini Kenya. Nadharia ya Ujinaishaji pamoja na nadharia ya Uchanganuzi Hakiki Usemi na Matini ziliongoza utafiti huu. Data ilikusanywa kupitia mahojiano ya ana kwa ana pamoja na hojaji. Mahojiano yalimwezesha mtafiti kupata data ya kutosha na halisi moja kwa moja kutoka kwa wahojiwa. Hojaji ilimwezesha mtafiti kukusanya data kwa urahisi katika maeneo mengi na kutoka kwa sampuli kubwa. Walengwa katika utafiti huu walikuwa wakaazi wa Mwimbi na Muthambi. Usampulishaji ulifanywa kimaksudi kwa kuhusisha machifu 5 wa kata 5 za Mwimbi na Muthambi na manaibu wa chifu 25 kutoka kata ndogo 25 za eneo hili. Watawala hao walichaguliwa kwa sababu walikuwa wenyeji wa eneo la utafiti na iliaminika kuwa wangetoa habari kamilifu kuhusu maswali ya utafiti. Sampuli nyingine ya Wazee 20 wenye umri wa miaka 70 na zaidi ilichaguliwa kimakusudi kwa kutumia mbinu ya kimtandao ili kutoa habari kuhusu michakato ya uundaji wa toponemia za shule za msingi katika eneo la Mwimbi na Muthambi. Sampuli ya wazee ilipatikana kwa urahisi kwa kuwa walikuwa wakipokea marupurupu maalum kutoka kwa serikali, na hivyo walijulikana katika vijiji vyao. Uchambuzi na uwasilishaji wa data ya utafiti huu ulitumia mkabala wa kimaelezo kulingana na madhumuni na swali la utafiti. Utafiti huu ulibainisha kuwa toponemia hutolewa kwa kuzingatia vigezo vya kimaumbile, kiuchumi na kijamii. Matokeo ya utafiti huu yatatoa marejeleo muhimu kwa watafiti wa baadaye watakaoshughulikia vipengele vya onomastiki katika lahaja ya Kimwimbi na Muthambi na lugha nyinginezo.
  • No Thumbnail Available
    Item
    Uhusiano wa Kifahiwa katika Leksia za Kîîtharaka: Mtazamo wa Leksika Pragmatiki
    (2022) Mwembu, Kimathi; Mugambi, Allan; Kinoti, Timothy M.
    Makala haya yanalenga kubainisha jinsi fahiwa zinavyohusiana katika leksia za Kîîtharaka kwa kuzingatia mtazamo wa leksika pragmatiki.Ubadili maana katika leksia mbalimbali husababisha kutokea uhusiano wa kifahiwa katika leksia moja, na kati ya leksia mbili au zaidi. Katika makala haya, ubadili maana unaozua uhusiano wa kifahiwa katika leksia za Kîîtharaka umeangaziwa. Data ya kimsingi kutoka wazungumzaji asilia wa Kîîtharaka, imechanganuliwa kwa kutumia nadharia ya Leksika-Pragmantiki. Matokeo yanabainisha kwamba ubadili maana ukitokea katika leksia za Kîîtharaka, mahusiano ya kifahiwa yafuatayo hutokea: uhusiano wa kipolisemia, kihomnimia, kisinonimia, kihaiponimia, kimeronimu na kiantonimu. Makala haya yanahitimisha kwamba, maana ya leksia huwa na uhusiano na maana nyingine ya leksia iyo hiyo au leksia nyingine tofauti. Pia, kuna mwingiliano baina ya maana kimatumizi na maana kimuktadha ya leksia.
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Umbuji wa Wahusika katika Ushairi wa Kiswahili: Mifano Kutoka kwa Diwani ya Jicho la Ndani (S.A. Mohamed, 2002).
    (2019-06) Kinoti, Timothy M.
    Suala la utunzi na uhakiki wa mashairi ya Kiswahili limejadiliwa kwa muda mrefu na washairi na wataalamu mbalimbali. Mjadala huu umejikita katika dhana na maana ya shairi la Kiswahili na iwapo lihakikiwe kwa kuzingatia kaida zilizowekwa na wanamapokeo au uhuru ulioibuliwa na wanamapinduzi. Hali hii imekinza kwa kiasi fulani uzingatiaji kikamilifu wa mbinu nyinginezo za kiubunifu za kulihakiki shairi la Kiswahili. Kati ya vipengele muhimu katika sanaa hii kongwe vilivyotelekezwa kiasi ni uteuzi wa wahusika, uchunguzi wa mazingira wanamopatikana na hisia wanazotumiwa na mshairi kuwasilisha, kama inavyosisitizwa katika Nadharia ya Ulimbwende. Kimsingi, jamii husawiriwa katika kazi za fasihi kupitia wahusika kwani ndio wawakilishi na viwakilishi vya hali halisi za wanajamii. Jinsi mshairi akatavyowateua na kuwasawiri wahusika wake katika mazingira mahsusi itaifanya hadhira kuyapenda au kuyachukia matendo, tabia na hali fulani za wanajamii waliowakilishwa na wahusika hao. Makala haya yananuiwa kubainisha dhima ya wahusika wa kishairi katika kujadili na kuhifadhi masuala ya kihistoria.
  • No Thumbnail Available
    Item
    Upambanuzi wa Miundo ya Toponemia katika Jamii: Mfano kutoka Jimbo Dogo la Maara nchini Kenya
    (2022) Mutegi, David Micheni; Mugambi, Allan; Kinoti, Timothy M.
    Makala hii imewasilisha uchunguzi uliofanywa kuhusu michakato na mbinu zilizotumika katika uundaji wa toponemia katika jamii. Lengo mahsusi la utafiti huu lilikuwa kupambanua miundo ya toponemia katika eneo la Mwimbi na Muthambi jimboni dogo la Maara. Maeneo haya yaliteuliwa kwa vile yalihusiana kilugha na kiutamaduni hasa katika suala la onomastiki. Nadharia ya Ujinaishaji ndiyo ilitumiwa kuongoza utafiti huu. Data ya utafiti huu ilikusanywa kwa kupitia kwa ya mahojiano ya ana kwa ana pamoja na hojaji. Mahojiano yalimwezesha mtafiti kupata data ya kutosha na halisi moja kwa moja kutoka kwa wahojiwa. Hojaji ilimwezesha mtafiti kukusanya data kwa urahisi katika maeneo mengi na kutoka kwa sampuli kubwa. Walengwa katika utafiti huu walikuwa wakaazi wa Mwimbi na Muthambi. Usampulishaji ulifanywa kimaksudi kwa kuhusisha machifu 5 wa kata 5 za Mwimbi na Muthambi na manaibu wa chifu 25 kutoka kata ndogo 25 za eneo hili. Watawala hao walichaguliwa kwa sababu wao ni wenyeji wa eneo hili walio na habari kuhusu maeneo yao ya utawala, na hivyo wangetoa habari kamilifu kuhusu maswali ya utafiti. Sampuli nyingine ya Wazee 20 wenye umri wa miaka sabini na zaidi walichaguliwa kimakusudi kwa kutumia mbinu ya kimtandao ili kutoa habari kuhusu michakato ya uundaji wa toponemia za shule za msingi katika eneo la Mwimbi na Muthambi. Sampuli ya wazee iliweza kupatikana kwa urahisi kwa sababu ndio wanaopata pesa za wazee na walijulikana katika vijiji vyao. Uchambuzi na uwasilishaji wa data ya utafiti huu ulitumia mkabala wa kimaelezo kulingana na madhumuni na swali la utafiti. Matokeo ya utafiti huu ni marejeleo muhimu kwa watafiti wengine watakaoshughulikia vipengele vya onomastiki katika lahaja ya Kimwimbi na Muthambi. Aidha, utafiti huu ulibainisha michakato mbalimbali ya uundaji wa toponemia katika jamii.
  • Loading...
    Thumbnail Image
    Item
    Usawiri wa Mwanasiasa wa Afrika Katika Ushairi wa Kiswahili
    (Chuka University, 2015-04) Kinoti, Timothy M.
    Utafiti huu ulishughulikia usawiri wa mwanasiasa wa Afrika katika ushairi wa Kiswahili. Kimsingi, mtafiti alichunguza jinsi washairi mbalimbali walivyowasawiri wanasiasa wa Afrika kiubunifu kwa lengo la kudhihirisha walivyobadilika kisiasa na kimaadili kutoka enzi za ukoloni hadi kipindi cha siasa za vyama vingi. Utafiti huu ulichukulia kuwa wanasiasa hawa hutekeleza wajibu mkubwa katika maendeleo ya mataifa yao na bara la Afrika kwa jumla. Uafikiaji wa malengo mbalimbali ya maendeleo kama vile Ruwaza ya 2030 nchini Kenya na uimarishaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kiasi kikubwa utategemea maamuzi ya kisiasa. Madhumuni ya utafiti huu yalikuwa kuchunguza nafasi ya ushairi wa Kiswahili katika uhifadhi wa historia ya mwanasiasa wa Afrika; kubainisha sifa za mwanasiasa wa Afrika kabla ya uhuru na kutathmini mabadiliko ya mwanasiasa wa Afrika baada ya uhuru kwa mujibu wa washairi wa Kiswahili. Mtafiti aliichukulia sauti ya mshairi kuwa sauti ya mwananchi ambaye ndiye huathiriwa na maamuzi na vitendo vya wanasiasa. Utafiti huu uliongozwa na Nadharia ya Ulimbwende iliyoasisiwa na William Wordsworth na Samuel Taylor Coleridge na Nadharia ya Baada-Ukoloni ambayo inahusishwa na kazi za Edward W. Said, Gayatri Chakravorty Spivak na Homi K. Bhabha. Utafiti huu ulifanyiwa maktabani ambapo mbinu ya sampuli ya kudhamiria ilitumiwa kuteua data kutoka kwa diwani teule. Uchanganuzi wa kimaelezo ulizingatiwa ambapo mashairi yaliyoteuliwa yalihakikiwa kwa mujibu wa madhumuni ya utafiti. Tasnifu hii imegawanywa katika sura sita. Sura ya kwanza imejumuisha utangulizi. Katika sura ya pili pana mwauo wa maandishi yanayohusiana na utafiti huu pamoja na misingi ya kinadharia. Sura ya tatu imeshughulikia mbinu za utafiti zilizotumiwa katika utafiti huu. Katika sura ya nne na tano, data imechanganuliwa, kuwasilishwa na matokeo kujadiliwa. Hatimaye, sura ya sita inatoa mahitimisho na mapendekezo kutokana na utafiti huu. Matokeo ya utafiti huu yamebainisha kuwa ushairi wa Kiswahili ni utanzu wa fasihi ulio na umuhimu mkubwa katika kuhifadhi matukio mbalimbali ya kihistoria. Kupitia uhifadhi huu, sifa na vitendo vya mwanasiasa wa Afrika vimebainika katika vipindi mbalimbali vya kisiasa. Imebainika kuwa mwanasiasa wa Afrika aliyeonekana kuwa mzalendo kabla ya uhuru alibadilika ghafla uhuru ulipopatikana na kuwa mkandamizaji wa umma alioapa kulinda. Aidha, wanasiasa walioonekana kutetea upatikanaji wa demokrasia ya vyama vingi hawajatekeleza demokrasia hiyo. Licha ya dosari zilizobainishwa na utafiti huu, ni dhahiri kuwa bara la Afrika bado lina wanasiasa wachache vielelezo ambao wanaweza kuigwa na wanasiasa wa wakati huu na wale wa baadaye. Matokeo ya utafiti huu yatawanufaisha wasomi wa Kiswahili, waandishi na washikadau wote wa masuala ya kisiasa barani Afrika na kwingineko ulimwenguni.

University of Embu | Library Website | MyLOFT | Chat with Us

© University of Embu Digital Repository. All Rights Reserved.