• Login
    View Item 
    •   Repository
    • Journal Articles
    • Articles: Department of Humanities
    • View Item
    •   Repository
    • Journal Articles
    • Articles: Department of Humanities
    • View Item
    JavaScript is disabled for your browser. Some features of this site may not work without it.

    Ubandikaji Majina na Majumlishi Memeto kama Mikakati ya Propaganda Katika Mdahalo wa Urais wa Kenya 2013

    Thumbnail
    View/Open
    Full text (301.1Kb)
    Date
    2018-12
    Author
    Wanyama, John K.
    Wandera, P. Simwa
    Metadata
    Show full item record
    Abstract
    Wanasiasa hutumia mbinu anuai kuelekeza uelewa wa suala la kisiasa; mikakati ya propaganda haswa ndiyo hutumika zaidi katika kampeni za kisiasa miongoni mwa wanadamu wote ulimwenguni. Shida kubwa ni kama jamii ya kistarabu na kibinadamu inaweza kuendelea kuthamini na kushiriki katika propaganda katika shughuli za uteuzi wa uongozi: kwani kwenye propaganda huwa kupiga chuku,uongo, chuki na mambo mengi ambayo ni kinyume na kutangamana kwa wanadamu kama washiriki wenza katika jamii. Kazi hii imetathmini namna mikakati miwili ilitumiwa na wagombea wa kiti cha urais nchini Kenya, mwaka wa 2013, kwa lengo la kushawishi wapiga kura na kujipa umaarufu. Utafiti uliongozwa na nadharia ya Uchanganuzi Hakiki wa Matini. Data ilikuwa kauli zilizoingiana na mikakati ya propaganda. Uchanganuzi ulizingatia maarifa ya kithamani, ya kimaudhui na kiuhakiki. Matokeo yalionyesha matumizi ya ubandikaji majina na majumlishi memeto. Tekniki hizi zilitumiwa na wagombea kwa lengo la kujijengea sifa njema huku wakilenga kubomoa sifa za wapinzani. Pia zilitumiwa kwa dhamira ya kuuza sera za vyama vyao huku wakidhamiria kudhalilisha sera za wapinzani. Kazi hii ni mchango adimu kwa taaluma ya uchanganuzi matini na mawasiliano ya kisiasa. Aidha ni ya manufaa kwa wanafunzi wa uchanganuzi matini, sayansi ya siasa na mawasiliano. Tafiti zaidi zinaweza kufanywa kuhusu mbinu nyingine kama vile balagha, na pia kuzingatia nadharia zingine tofauti zinazohusu uchanganuzi wa matini.
    URI
    http://repository.embuni.ac.ke/handle/123456789/4158
    Collections
    • Articles: Department of Humanities [35]

    University of Embu©
    Contact Us |
    Designed by 
    Atmire NV
     

     

    Browse

    All of RepositoryCommunities & CollectionsBy Issue DateAuthorsTitlesSubjectsThis CollectionBy Issue DateAuthorsTitlesSubjects

    My Account

    LoginRegister

    University of Embu©
    Contact Us |
    Designed by 
    Atmire NV